JINSI YA KUBADILI VERSION YA SIMU YAKO ROOT REQUIRED

As salaam aleikum Mswahili mwenzangu matumaini yangu uko poa kama mimi Alhamdulillah, leo tuangalie jinsi ya kubadilisha Version ya simu yako ya android wenda ukajiuliza kwanini nibadilishe Version ya android yangu naam inabidi tubadilishe kwasababu kuna app za muhimu wakati mwingine tunazihitaji lakini kutokana na version za simu zetu kuwa ni toleo la zamani tujikuta tunakosa uhondo huo. twende kwenye mada moja kwa moja tusipoteze muda sana, kama utakuwa na swali utaniuliza katika sanduku la maoni


Hatua ya kwanza download app inaitwa Root browers kutoka playstor nenda moja kwa moja na link hiyo hapa Download.

Baada ya kuifungua utaona files zimetokea nyingi hapo teremka chini na tafuta /angalia file lililoandikwa *System*

Fungua humo na teremka chini utaona kiji file kimeandikwa Build.prop
Angalia hicho maana vipo viwili kengine kanaitwa Build.prop.bak

Bonyeza Build.prop kisha itafunguka na options tano hapo angalia palipo andikwa RB text Editor

Ukisha bonyeza hapo itafunguka na utaona detail zote za simu sasa hapo utafanya chaguo lako kama unataka kubadili builder number, manufactures,  na mengineyo kwa version utashuka chini 
 kisha utaangalia palipo andikwa ro.build.version.release=[hapa itakuwepo version original ya simu kisha utaifuta na kuweka mpya]


NOTE; Hakikisha unaweka version isiyo zidi 7 usidhidishe zaidi ya hapo ili kuweka simu yako katika Latest isiwe imepitiliza italeta shida

kisha ukimaliza kufanya mabadiliko hayo utasevu kwa kubonyeza icon ya sevu iliyopo juu kabisa mkono wa kulia kialama chake kipo kama mfano wa hichi ki emoj 🏥

 kisha restart simu yako na nenda kaanglie version mpya uliyoweka katika settings kisha about phone
 na utaweza kudownload app bila kikomo kwa kutokuwa na kizuizi cha version

Kuna apps ambazo zinarun kwenye version latest tu, kwahiyo ukiweka version latest apps latest zitakubali. 

Kwa mfano Recharge king haiwezi kurun kwenye W3 tecno ila inarun kwenye k7 na k9 lakini ukibadilisha version kwenye w3 na kuweka 7 itarun bila shida.

Imeandikwa na Riyadi Bhai Sambaza makala kama ilivyo kama unahitaji kukopi makala hii soma hapa Copyright Policy Zingatia sheria za Blog hii Ahsante kwa Kutembelea Swahili Tech

6 Comments

Je unamaoni kuhusu makala uliyoisoma dondosha maoni yako hapa