Kwa mtoto wangu mdogo wa kike Ghufairah,
Nataka kukuambia mambo mengi sana
Tazama Baba ameishi maisha marefu, na amepitia mambo mengi sana
Kwa hiyo naomba ujifunze kutoka kwangu
Makosa, na kufaidika na yale ambayo nimeona
Kwa matumaini kwamba utakuwa vizuri sana
Bora kuliko kila kitu ambacho nimekuwa
Ewe mtoto wangu mpendwa, jua kwamba kuna Mungu mmoja tu,
Na Yeye Subhanahu wataala anastahiki zaidi mapenzi yenu yote
Ameumba kila kitu na ana ujuzi wa kila kitu
Basi usimfanyie mshirika, na mcheni tu Yeye
Na fahamu kwamba mnapofanya dhambi ni lazima mrejee kwake na mkumbuke
Kwa kushikilia kamba yake Mola, itakuongoza tu kuelekea Jannah
Mahali pa raha zote, ambapo mtakaa na kukaa milele
Katika kampuni ya watu bora ambayo mizani ya haki imewahi kupima
Ewe mtoto wangu mpendwa, jua kwamba Mwenyezi Mungu ana haki juu yako na mimi.
Kwanza kabisa, anzisha yako Swalah, na usiiache ipite mpaka ufe
Kwa hivyo omba kila sala kana kwamba ni nafasi yako ya mwisho kusema kwaheri
Na kamwe usione aibu kuinua mikono yako na kumwita nakumtaka msaada
Ewe mtoto wangu wa kike, wewe ni mrembo kuliko vile utakavyowahi kujua
Na hauitaji mtu yeyote kukuambia kuwa wewe ni mrembo.
Hayo ni kwa sababu Mola wako amekufanya hivyo
Basi iheshimu zawadi hii ambayo Mwenyezi Mungu Amekutunuku
Wala usidhihirishe Aliyo yazuilia ila kwa wale Aliowachagua
Na ujue kwamba hijabu hii unayoipenda Kuvaa ni zaidi ya nguo tu
Ni ukumbusho kwa ulimwengu kwamba wewe Ni zaidi ya kile wanachokitazama
Akili, mwili na roho isiyodhibitiwa na kila kisanduku kidogo cha media
Kabla ya kila rafiki na mwenendo,
Unapaswa tu kuwa na wasiwasi juu ya kumvutia Mungu Mmoja
Na kisha baada ya hayo mama yako anastahili upendo wako wote,
Alikubeba kwa muda wa miezi 9 na kukutunza kwa upendo murua
Kwa hivyo mtendee wema kwa rehema na heshima hata unapofikiri amekosea
Na ninaahidi tutajitahidi tuwezavyo kukulea katika nyumba yenye upendo
Nitakuweka miguuni mwangu usiku na kukusomea hadithi hadi ulale
nitashiriki nawe kuijua historia ya Musa na Bani Isreal
Nitakuambia kuhusu Chewa ambaye alimmeza nabii Yunus mzima mzima
Na mchwa aliyezungumza na Suleimani kutoka ndani kabisa ya shimo
Tutajifunza yote kuhusu maswahaba, na kukariri kila jina la mmoja wao
Nitakuambia kuhusu Bilal ibn Rabah,
Na kukuonyesha kuwa ukoo wetu ni sawa Tutapenda hadithi ya Mtume wetu, kila wakati
Na tutalia kila wakati tunapofika mwisho Nataka kuwa rafiki yako bora, nataka kuwa yule ambaye unamtegemea Nataka unipigie kutoka shuleni uniambie Umesahau kazi yako ya nyumbani,tena
Ninataka kukupeleka kwenye safari, nataka uone ulimwengu
Nataka kushikilia mkono wako mbele ya Kaaba na kukuonyesha jinsi gani mbingu inavyoonekana duniani
Ninataka kukufundisha kuendesha baiskeli, nataka kukufundisha kuendesha gari pia.
Nataka kukufundisha kuwafukuza huko Wapenda mali hawatakufikisha mbali
Kwa sababu watu wengine ni masikini, kitu pekee wanalicho nacho ni pesa,
Ninataka kukufundisha kuridhika.
Mwenyezi Mungu na mimi tunaahidi kuwa utakuwa na furaha daima
Kwa sababu ikiwa marais, mawaziri wakuu, wafalme na malkia wote
Walijua baraka za Uislamu, Wakweli pia wangetupigania kwa ajili ya Dini hii uislamu.
Ninataka kuwa karibu yako nikufariji utakapoota ndoto mbaya;
Ninataka kukuambia ukweli kuhusu Halloween
Kwa nini hatuvai kama masheytwan,
Lakini bado nitakununulia pipi zaidi ya unazoweza kula Nataka nikufundishe kwamba unavuna ulichopanda,
Na kwamba kazi ngumu na mapambano yatakusaidia kukua Ninataka kukufundisha kutorudi nyuma kutokana na changamoto Na uaminifu huo ndio njia pekee ya kwenda mbele.
Nataka kukufundisha Qur'an, nataka kukufanya uipende Qur'an
Nataka uihifadhi moyoni mwako,
Chukua hatua na uione dunia nzima kupitia Qur'an
Nataka ufahamu makatazo ya Mwenyezi Mungu na maamrisho yake
Na kufuata kwa ubora wako kuliko mafundisho yoyote
Mfano, mjumbe wake Aleiyh salatu wasalaam
Na siku moja, naomba kwa mola wako na utapata upendo wa kweli, lakini sio tu kwa mwanaume yeyote
Lakini kwamba utaolewa na mwanamume ambaye pia ana mapenzi na uislam
Hivyo kama unataka mwanaume kama Muhammad, Inakubidi uwe mwanamke kama Khadija
Msaidizi wa kwanza wa jambo hili la uislamu na mama kwa waumini
Kuwa na ujasiri kama wa Nusaybah, usirudi nyuma katika ukweli
Tetea kile unachoamini hata wakati ulimwengu wote utasimama kukupinga.
Kuwa na elimu kama ya Aisha, kuwa mwanachuoni wa dini hii
Ponya watu kutokana na imani potofu kwa sababu Ujinga ni ugonjwa
Uwe na uchamungu wa Hafsa, na umuweke Mwenyezi Mungu juu ya mawazo yako
Funga mchana na uswali usiku, ili kuisaidia nafsi yako kukaa sawa
Kuwa na heshima ya Balqis, ifanye dunia ikutendee wema kwa utu wako
Wanapokuona mitaani,wajulishe kuwa wewe ni malkia
Kuwa na nguvu za Sumayya na subira kama ya Hajar,
Kuwa imara kama Maryam, tawakkul kama mama yake Musa
Na mambo yanapokuwa magumu, uwe kama mke wa firuan
Ambatanisha moyo wako na Jannah, na usiiache kamwe ndoto hii.
Maana wewe ni mpenzi wa kweli kwangu, kama Fatima kwa Nabii wetu
Mwenyezi Mungu akubariki kwa utulivu, kuanzia sasa hadi milele. Ameen
Mtoto wangu wa kike, nimekuleta katika ulimwengu wenye mambo mengi sana
Ambapo ukweli unaweza kuumiza, na uwongo unaweza kung'aa kama lulu
Dunia hii ni pepo kwa wale ambao wameuza roho zao
Na ni gereza kwa wale wanaoshikilia kanuni hii ya maadili
Mtoto wangu wa kike, nakuahidi hilo.
Niko hai nitajitahidi kukufanya utabasamu
Nitaenda maili nyingi za ziada kwajili ya mtoto wangu Ghufairah, lakini tambua
Kwamba dunia hii imejaa majaribu
Hiyo itabidi upitie tu, na fahamu ya kuwa wewe huna wakumtegemea ila Mwenyezi Mungu.
Tambua ya kwamba Mwenyezi Mungu ni zaidi ya msaada kwako
Ninakuombea kila wakati, kwa hivyo tafadhali niombee pia,
Muombe Mwenyezi Mungu anisamehe madhambi yangu, na alijaze kaburi langu Nuru
Lakini nakuahidi, Jannah tutaendelea na mchezo wetu mdogo wa kukimbizana kati ya Baba na msichana wake mdogo.
Nakupenda sana Binti Yangu Ghufairah
Hisia zangu kwa Bint yangu wa kipekee
Ibrahim Riyad Ruwehy
0 Comments
Je unamaoni kuhusu makala uliyoisoma dondosha maoni yako hapa