as salaam aleikum ndugu zangu wasomaji wa blog hii nimeshindwa kuwa hewani kwa kitambo kidogo kutokana na pirikapirika za kusaka mkate wa siku sasa nimerudi tena kidogo kuwajulia hali natumaini ni wazima kabisa tujifunze kila siku tujifunze kila kitu.
Ni rahisi sana kufahamu passwords za network zote za Wi-Fi ambazo kompyuta yako ya Windows ilishawahi kuungwa kwa kutumia Command Prompt (cmd) inayopatikana katika mfumo endeshi wa Windows.
Mara nyingi watu wanaohusika na IT au kitengo cha IT ndio wanaohusika zaidi na utoaji wa password za wifi katika maeneo yetu ya kazi, mashuleni au vyuoni. Mara nyingi huwa wanazificha passwords hizi hata kwa watumiaji wa kompyuta wa ndani.
Kama wewe ni mmoja wanaokumbwa na kadhia hii kutoka kwa IT wa ofisini au chuoni kwenu usitie shaka, hapa ndio mahala pake. Leo nitakuelekeza jinsi ya kupata password za wifi networks zote ulizowahi kujiunga kwa urahisi zaidi.
Kila mara tunapojiunga na WLAN katika kompyuta zetu, kuna profile maalumu kwa ajili ya WLAN hiyo huwa linatengenezwa katika kompyuta zetu bila ya sisi kufahamu. Profile hilo linakuwa na taarifa zote za muhimu zinazohusiana na network hiyo.
Njia hii inatumika hata kama upo Offline na haujajiunga kabisa katika network hiyo kwa wakati huo.
Jinsi ya kufahamu password za WiFi Network
Fungua Command Prompt kama Administrator, bonyeza Windows + X kufanya hivyo
Hatua inayofuata ni sisi kutambua profile zote za wlan zilizowahi kuhifadhiwa katika kompyuta zetu. Andika komandi ifuatayo katika cmd kisha bonyeza enter: netsh wlan show profile
Komandi hiyo itakuonyesha profile zote zilizowahi kuhifadhiwa katika kompyuta yako.
Baada ya kuona profile zote za WLAN ulizowahi kuunganishwa nazo, sasa ni wakati wa kuangalia password kwa kila pofile kwa kuandika komandi: netsh wlan show profile WiFi-name key=clear
Badilisha sehemu ya WiFi-name na weka jina la wifi unayotaka kuona password yake
Katika sehemu ya security settings, katika kipengere cha ‘key content’ utaona password za wifi husika.
JINSI YA KUPATA PASSWORDS ZA WI-FI KWA KUTUMIA CMD
Riyadi
June 18, 2018
0
Comments
Tags
Related Article
0 Comments
Je unamaoni kuhusu makala uliyoisoma dondosha maoni yako hapa