JINSI YA KUWEKA TANGAZO MNATO [STICKY ADS] KATIKA BLOG YAKO


As salaam aleikum ndugu zangu wasomaji wa blog hii, kutokana na ombi la ndugu yetu Mfangavo kuhusu kujua jinsi ya kuweka sticky Ads basi nimeonelea niandae makala kamili ili tunufaike sote kwa pamoja wenda na wewe ulikuwa mmoja miongoni mwa watu waliohangaika kujaribu kufahamu jambo hili ila jitihada zako zikagonga ukuta, basi leo wacha nikupe suluhisho la jambo lako hilo kuwa makini katika usomaji wako ili upate kunielewa vema.

Hapa chini nimekuwekea code ambazo utaziweka katika blog yako katika upande wa Layout




<div style="left:0;position: fixed;text-align:center;bottom: 0px;width:100%;z-index:9999;"><center><a href="weka link ya tangazo lako">
<img src="weka code ya adsense hapa/ weka link ya picha ya tangazo lako">
</a></center></div>



Twende sawa sasa hizo code unazoziona hapo juu ndio code tutacazo zitumia katika kukamilisha jambo letu hili copy code hizo  kisha nenda katika Layout ya blog yako kisha bonyeza Add a Gadget kama uovyoona katika picha hapo chini
 Kisha chagua Gadget iliyoandikwa HTML/JavaScript kama unavyoona pichani hapo chini, hapo ndio tutakapozikweka code zetu
 Kisha utaona uwanja ambao hauna kitu pacte/pachika code zako ulizozikopi hapo juu kwenye sehemu ya Title usiandike kitu, edit/rekebisha code zako kisha bonyeza sehemu iliyoandikwa save
 Shabbash mpaka kufikia hapo utakuwa umefanikiwa kuweka Tangazo mnato/mgando katika blog yako hata kama mtu atafungua post ataliona tangazo hilo kama unavyoona pichani hapa chini


Bila shaka nimejitahidi kurahisisha katika kuelezea Jambo letu hili kama utakuwa kuna sehemu hujaelewa basi unaweza kuniachia maoni yako hapo chini nami nitajitahidi kukusaidia kadri nitakavyoelewa

makala hii Imeandikwa na Riyadi Bhai Sambaza kama Ilivyo kama unahitaji kukopi makala zetu zilizopo katika blog hii wasiliana nami kwa email RiyadiBhai@gmail.com


8 Comments

  1. doooh, ahsante sana kaka, nmefanikiwa kuweka, mungu akujaalie uwe na moyohuo huo wakusaidia

    ReplyDelete
    Replies
    1. Karibu sana ndugu, usisahau kushare link ya blog yetu na kutufuata katika mitandao yetu ya kijamii. Kama utakuwa na jambo lolote usisite kuwasiliana nasi

      Delete
  2. weka link ya tangazo lako (link kama seebait unaweka yote si ndio)
    weka code ya adsense hapa/ weka link ya picha ya tangazo lako (hapo napo sijapaelewa kabisa naomba ufafanuzi kidogo)

    ReplyDelete
    Replies
    1. Kama unataka kuweka code za seebait au Adsense au mfano wa hizo pale kwenye link ya tangazo weka tu alama ya reli kisha kwenye link ya picha ya tangazo ndio pachika code za tangazo lako la adaense au seebait au mfano wa hayo.

      Bila shaka nimejibu swali lako vema

      Delete
    2. umejibu haswa ila shida inakuja moja nime weka matangazo i mean code zile za seebait ila sasa tatizo linakuja kwenye kuonekana maana nakumbuka ulisema kama ikionekana tangazo imeeandikwa seebait na yule dada means haupokei chochote kile na sasa mbona inaonekana banner moja tu mda mwingine mbili hebu angalia https://habarizero.blogspot.com/ kisha uniambie au ndo hivyo huwa inaonekana mpaka wapate matangazo maana ndo nime sajili juzi tu hata week bado na sija fikisha hata views laki moja

      Delete
    3. Ni kweli katika moja ya makala zangu nakili kuandika ivo ila kwa sasa hata ikiwa banner ile wanalipa kwa USD 0.60 kwa user 1000 na kuhusu kubadilika huwa inategemea wao kupata matangazo

      Delete
  3. This comment has been removed by a blog administrator.

    ReplyDelete
  4. Brother naomaba unipe namba yako au nicheki 0717247313 nikupigie unieleweshe

    ReplyDelete

Je unamaoni kuhusu makala uliyoisoma dondosha maoni yako hapa