As salaam aleikum ndugu zangu wasomaji wa blog hii, kutokana
na ombi la ndugu yetu Mfangavo kuhusu kujua jinsi ya kuweka sticky Ads basi
nimeonelea niandae makala kamili ili tunufaike sote kwa pamoja wenda na wewe
ulikuwa mmoja miongoni mwa watu waliohangaika kujaribu kufahamu jambo hili ila
jitihada zako zikagonga ukuta, basi leo wacha nikupe suluhisho la jambo lako
hilo kuwa makini katika usomaji wako ili upate kunielewa vema.
Hapa chini nimekuwekea code ambazo utaziweka katika blog
yako katika upande wa Layout
<div style="left:0;position: fixed;text-align:center;bottom: 0px;width:100%;z-index:9999;"><center><a href="weka link ya tangazo lako">
<img src="weka code ya adsense hapa/ weka link ya picha ya tangazo lako">
</a></center></div>
Twende sawa sasa hizo code unazoziona hapo juu ndio code
tutacazo zitumia katika kukamilisha jambo letu hili copy code hizo kisha nenda katika Layout ya blog yako kisha bonyeza Add a Gadget kama uovyoona katika picha hapo chini
Kisha chagua Gadget iliyoandikwa HTML/JavaScript kama unavyoona pichani hapo chini, hapo ndio tutakapozikweka code zetuKisha utaona uwanja ambao hauna kitu pacte/pachika code zako ulizozikopi hapo juu kwenye sehemu ya Title usiandike kitu, edit/rekebisha code zako kisha bonyeza sehemu iliyoandikwa save
Shabbash mpaka kufikia hapo utakuwa umefanikiwa kuweka Tangazo mnato/mgando katika blog yako hata kama mtu atafungua post ataliona tangazo hilo kama unavyoona pichani hapa chini
makala hii Imeandikwa na Riyadi Bhai Sambaza kama Ilivyo kama unahitaji kukopi makala zetu zilizopo katika blog hii wasiliana nami kwa email RiyadiBhai@gmail.com
8 Comments
doooh, ahsante sana kaka, nmefanikiwa kuweka, mungu akujaalie uwe na moyohuo huo wakusaidia
ReplyDeleteKaribu sana ndugu, usisahau kushare link ya blog yetu na kutufuata katika mitandao yetu ya kijamii. Kama utakuwa na jambo lolote usisite kuwasiliana nasi
Deleteweka link ya tangazo lako (link kama seebait unaweka yote si ndio)
ReplyDeleteweka code ya adsense hapa/ weka link ya picha ya tangazo lako (hapo napo sijapaelewa kabisa naomba ufafanuzi kidogo)
Kama unataka kuweka code za seebait au Adsense au mfano wa hizo pale kwenye link ya tangazo weka tu alama ya reli kisha kwenye link ya picha ya tangazo ndio pachika code za tangazo lako la adaense au seebait au mfano wa hayo.
DeleteBila shaka nimejibu swali lako vema
umejibu haswa ila shida inakuja moja nime weka matangazo i mean code zile za seebait ila sasa tatizo linakuja kwenye kuonekana maana nakumbuka ulisema kama ikionekana tangazo imeeandikwa seebait na yule dada means haupokei chochote kile na sasa mbona inaonekana banner moja tu mda mwingine mbili hebu angalia https://habarizero.blogspot.com/ kisha uniambie au ndo hivyo huwa inaonekana mpaka wapate matangazo maana ndo nime sajili juzi tu hata week bado na sija fikisha hata views laki moja
DeleteNi kweli katika moja ya makala zangu nakili kuandika ivo ila kwa sasa hata ikiwa banner ile wanalipa kwa USD 0.60 kwa user 1000 na kuhusu kubadilika huwa inategemea wao kupata matangazo
DeleteThis comment has been removed by a blog administrator.
ReplyDeleteBrother naomaba unipe namba yako au nicheki 0717247313 nikupigie unieleweshe
ReplyDeleteJe unamaoni kuhusu makala uliyoisoma dondosha maoni yako hapa