FAHAMU MUDA WA TOVUTI/BLOG KUANZA KUKULIPA

As salaam aleikum mpendwa karibu katika tovuti yako pendwa tuendelee kupashana habari, unajua kuna watu wamesimuliwa kuhusu kupata pesa katika blog ivo wakaona ni jambo la dakika kadhaa tu ataweza kupata pesa, ni kweli unaweza kupata pesa nyingi mno lakini sio rahisi na kwa muda mfupi ivo blogging inahitaji kujitoa kimwili na kiakili, utatakiwa kutumia muda rasilimali pesa na watu ikibidi ivo kabla ya kufungua blog inabidi ujipange kiasi japo kuna watu husema ni bure lakini sio bure kama wewe unavyodhani sababu kuna vitu lazima ugharamie kama utahitaji pro theme lazima ununue na sio chini ya U$D 10 kama utahitaji domain kama www.swahilitech.net lazima ununue pia, nisikuchoshe sana ebu twende katika somo tulilolikusudia.


  1. Kuna tovuti aina ngapi zinazoweza kukulipa? 


Tovuti yoyote ile inaweza kukuingiazia kipato ni kutokana na malengo yako.Naweza kuzigawa tovuti zinazoweza kukuingizia kipato katika sehemu mbili,


  • Tovuti inayofunguliwa ikiambatana na biashara uliyo nayo(mfano una kampuni/duka hapo ndio unalifungulia tovuti)
  • Tovuti inayofunguliwa isiyoambatana na biashara(hauna kampuni/duka) kama hii swahilitech.net


Hapa nitazungumzia aina ya pili hapo juu(ambayo hauna duka/kampuni).Ili uweze kupata kipato katika aina hii ya pili ya tovuti itakubidi uzingatie masuala yafuatayo;

  • Tovuti yako lazima ikidhi mahitaji ya watu(yakiwa mahitaji ya lazima ni vizuri zaidi)
  • Iwe na muonekano mzuri
  • Iweze kufunguka haraka
  • Iendane na hadhira unayokusudia
  • Iweze kuonekana vizuri katika simu za mkononi/zenye screen ndogo
  • Tovuti ijitangaze yenyewe
  • Tovuti uitangaze katika mitandao ya kijamii bure au hata kwa kulipia
  • Tovuti uifanyie SEO
  • Lazima uisimamie mwenyewe
  • Pata ushauri pindi inapohitajika
  • Fanya market/keywords research kwa bidhaa/huduma unayotoa.


Muda unatofautiana kutokana na vitu hivi;
1.Aina ya tovuti
2.Mtaji uliotumika/investment

Hapa nitazungumzia aina ya tovuti. Tovuti zinazofunguliwa kutoa huduma fulani ambayo ni muhimu na lazima hizi zitachukua muda mfupi kuanza kukulipa,ukilinganisha na tovuti zitazofunguliwa kutoa huduma ambazo sio za lazima. Mfano umefungua tovuti ya kuuza bidhaa hii inaweza kuanza kukulipa ndani ya mwezi mmoja toka uifungue,Kwa hiyo muda wa kuanza kukulipa inatokana na muda wako katika tovuti hiyo.Usipoifanyia online/offline promotion haiwezi kukulipa kabisa.

kila kitu ni juhudi ili uweze kufanikiwa katika jambo hilo ni lazima ujitolee kwa hali na mali. 

matumaini yangu umepata mwanga japo kidogo kuhusu makala yetu hii sambaza na marafiki wengine wajue jambo hili.

0 Comments

Je unamaoni kuhusu makala uliyoisoma dondosha maoni yako hapa