FAHAMU SIMU AMBAZO HAZIFAI KU-ROOT KWA KUTUMIA KINGO ROOT
RiyadiJune 17, 20170
Comments
Kingo Root ni moja ya njia maarufu ambayo inatumiwa na watu wengi ili
ku-root simu zao. Lakini hii njia huwa haifanyi kazi kwenye kila simu.
Zipo baadhi ya simu ambazo hazifai kabisa kuroot kwa kutumia Kingo Root
HTC
Simu nyingi za aina ya HTC huwa hazifai kabisa ku-root kwa kutumia Kingo
root. Moja ya sababu inayo sababisha hizi simu zisifae kuroot kwa
kutumia kingo root ni ulinzi mkali ambao HTC wanaweka kwenye simu zao. Locked Bootloader na S-ON
ni ulinzi ambao HTC wanaweka kwenye simu zao ili kuzuia mtumiaji
asiweze ku-access au ku-modify system files. Ndio maana ili uweze
ku-root simu za HTC inabidi kwanza unlock bootloader na uhakikishe S-ON
ipo S-OFF. Tazama picha chini kuelewa zaidi.
SAMSUNG
Kama ilivyo HTC, Samsung nao wanaweka ulinzi mkali ambao unazuia simu
zao kuwa ngumu sana ku-root kwa kutumia Kingo Root. Zipo baadhi ya simu
za Samsung ambazo zinakuja na locked bootloader. Ukiachana na locked
bootloader, Samsung wana ulinzi mwingine mkali unao julikana kama Knox.
Knox security inamzuia mtumiaji asije modify au ku-access system files.
Ili uweze ku-root simu za samsung basi ni lazima Knox security iwe
turned off. Tazama picha chini ili kuelewa zaidi
HUAWEI
Huawei pia wapo kwenye hili kundi ambalo huwezi ku-root simu zao kwa
kutumia kingo root. Zipo baadhi ya simu za huawei ambazo utaweza ku root
kwa kutumia kingo root lakini ni chache sana. Huawei pia ana lock
bootloader za simu zao na kusababisha kuwa vigumu sana ku-root simu za
huawei. Sio kwamba Huawei hawa ruhusu simu zao kuwa rooted, jibu ni
kwamba Huawei wana ruhusu simu zao kuwa rooted lakini wanapenda ufwate
utaratibu maalumu walioweka ili endapo uta root simu yao basi ujue
kabisa utakuwa umepoteza warranty yako
0
Comments
Je unamaoni kuhusu makala uliyoisoma dondosha maoni yako hapa
0 Comments
Je unamaoni kuhusu makala uliyoisoma dondosha maoni yako hapa