FAHAMU SIMU AMBAZO HAZIFAI KU-ROOT KWA KUTUMIA KINGO ROOT

Kingo Root ni moja ya njia maarufu ambayo inatumiwa na watu wengi ili ku-root simu zao. Lakini hii njia huwa haifanyi kazi kwenye kila simu. Zipo baadhi ya simu ambazo hazifai kabisa kuroot kwa kutumia Kingo Root

HTC

Simu nyingi za aina ya HTC huwa hazifai kabisa ku-root kwa kutumia Kingo root. Moja ya sababu inayo sababisha hizi simu zisifae kuroot kwa kutumia kingo root ni ulinzi mkali ambao HTC wanaweka kwenye simu zao. Locked Bootloader na S-ON ni ulinzi ambao HTC wanaweka kwenye simu zao ili kuzuia mtumiaji asiweze ku-access au ku-modify system files. Ndio maana ili uweze ku-root simu za HTC inabidi kwanza unlock bootloader na uhakikishe S-ON ipo S-OFF. Tazama picha chini kuelewa zaidi.

SAMSUNG

Kama ilivyo HTC, Samsung nao wanaweka ulinzi mkali ambao unazuia simu zao kuwa ngumu sana ku-root kwa kutumia Kingo Root. Zipo baadhi ya simu za Samsung ambazo zinakuja na locked bootloader. Ukiachana na locked bootloader, Samsung wana ulinzi mwingine mkali unao julikana kama Knox. Knox security inamzuia mtumiaji asije modify au ku-access system files. Ili uweze ku-root simu za samsung basi ni lazima Knox security iwe turned off. Tazama picha chini ili kuelewa zaidi

HUAWEI

Huawei pia wapo kwenye hili kundi ambalo huwezi ku-root simu zao kwa kutumia kingo root. Zipo baadhi ya simu za huawei ambazo utaweza ku root kwa kutumia kingo root lakini ni chache sana. Huawei pia ana lock bootloader za simu zao na kusababisha kuwa vigumu sana ku-root simu za huawei. Sio kwamba Huawei hawa ruhusu simu zao kuwa rooted, jibu ni kwamba Huawei wana ruhusu simu zao kuwa rooted lakini wanapenda ufwate utaratibu maalumu walioweka ili endapo uta root simu yao basi ujue kabisa utakuwa umepoteza warranty yako

0 Comments

Je unamaoni kuhusu makala uliyoisoma dondosha maoni yako hapa