Uzinduzi wa iPhone xs wapelekea Simu za iPhone 6, SE, X zisitatengenzwa tena

Kufuatia uzinduzi wa simu za iPhone kwa mwaka 2018 ambazo zinahusisha iPhone XS, iPhone XS Max na iPhone XR, imebainika kwamba sasa simu zake nyingi za modeli zilizopita, ikiwamo iPhone X, sasa hazitatengezwa tena.
Simu hizo zilizoondolewa sokoni, na ambazo pia zimefutwa rasmi katika tovuti ya Apple ni pamoja na iPhone 6S na iPhone SE, hiyo ikimaanisha kuwa sasa huwezi tena kununua iPhone yenye sehemu ya kuchomeka spika za masikioni ukubwa wa milimita 3.5.

Mojawapo ya iPhone ambazo Apple wametangaza kuachana nazo na hatua hyo ni kwamba unaweza kununua hizo simu katika maduka mengine na si katika tovuti rasmi ya Apple.
Habari njema kwa mashabiki ni kwamba, Apple bado inauza iPhone 7, iPhone 8 na iPhone 8 Plus katika tovuti yake hivyo kuwa bidhaa pekee za iOS unazoweza kuzinunua moja kwa moja kutoka kwao.

Na pia kama ulikuwa unasubiri kuchaji simu yako mpya ya iPhone katika AirPower mat, utapaswa kusubiri hadi Septemba 21 mwaka huu wakati Chaji Qi isiyotumia waya itakapotolewa rasmi kwingineko duniani baada ya kuzinduliwa Septemba 14.

0 Comments

Je unamaoni kuhusu makala uliyoisoma dondosha maoni yako hapa