SEEBAIT YACHAGULIWA KUWANIA TUZO ZA SOUTHERN START UPS AWARDS

Seebait.com, moja ya makampuni yanayoongoza katika matangazo ya mtandaoni, imechaguliwa kuwania nafasi ya kuiwakilisha Tanzania katika tuzo zijulikanazo kama Southern Africa Startup Awards.



Taarifa iliyotolewa na msemaji wa Seebait Jijini Dar es Salaam, ilisema kuwa Seebait imechaguliwa kati ya washindani wengine 3200.

Alisema walichaguliwa na majaji na wataalamu kuwa miongoni mwa makampuni mengine ili wapate nafasi ya kuiwakilisha Tanzania katika kipengele kimoja kati ya 14 katika Tuzo hizo  zitakazofanyika Novemba 21 na 22 mwaka huu huko Johannesburg, Afrika Kusini.

Alitoa rai kwa watanzania wawapigie kura kwa wingi ili Seebait ipate nafasi hiyo muhimu  katika Tuzo hizo za kwanza kuandaliwa na Southern African Start Up Awards.

Kwa watakaotaka kupiga kura, wanatakiwa kwa mujibu wa msemaji  kutembelea


Alisema upigaji kura umeanza rasmi na zoezi hilo litakamilika siku ya  Ijumaa Septemba 4 na kuwa matokeo yatatangazwa na jopo la majaji waliochaguliwa kila nchi ili kupata washindani wa kila kipengele ambao watawakilisha nchi zao katika ngazi za kanda na pengine katika hatua ya dunia.

Kwa mujibu wa Southern African Start Up Awards, kutakuwa na kipengele cha Shirika ambalo ni Chaguo la watu (People’s Choice Category).

“Matokeo yatatangazwa na wabia wa Southern Africa Start Up Awards mara baada ya upigaji kura kukamilika,” alisema.

Seebait ilianzishwa mwaka 2015 kama kiunganishi kati ya watoa matangazo na wenye majukwaa mbalimbali kama tovuti na blogs ili kuhakikisha watangazaji wanapata jukwaa kubwa zaidi la kutangaza bidhaa au huduma zao na wenye majukwaa haya wanapata wasaa mzuri wa kuandaa maudhui bora kwa watembeleaji wao, pia wakitangaza bidhaa na huduma mbali mbali kupitia majukwaa yao  na kupata stahiki zao vikamilifu.

seebait.com inashikilia nafasi ya kwanza kwa Tanzania kwenye chati za Global start up ranking,


Tembelea www.seebait.com kujua mengi.

0 Comments

Je unamaoni kuhusu makala uliyoisoma dondosha maoni yako hapa