MAMBO 5 YANAYOKUFELISHA KATIKA SAFARI YAKO YA KUBLOGGING

As salaam aleikum ndugu yangu blogger mwenzangu au hata msomaji wangu natumaini wewe ni mzima mimi pia alhamdulillah, Katika zama hizi watu wengi sana wanamiliki blogs, za personal, entertainment au matangazo mbali, kila mtu akiwa na dhamira tofauti akilini mwake. Lakini sio Kila Blog inayoanzishwa inadumu, wengi hushindwa kufika mbali na hatimaye blogs zao hufa au kukosa wafuatiliaji.

Zifuatazo ni miongoni mwa sababu zinazosababisha Blog nyingi Kutofanikiwa:-


1.Kukosa Content zako Mwenyewe, hatimaye kuanza Ku Copy na Ku Paste.

Hili ni jambo ambalo Bloggers wengi wa Hapa kwetu Tanzania Wamelizoea, Ndio maana utakuta habari au makala ileile imeandikwa na Bloggers zaidi ya watano bila kubadilishwa kitu, hii hupunguza taswira ya umakini toka kwa wafuatiliaji wako.

2. Kukosa Ufuatiliaji katika Blogs/Sites zenye Muingiliano na Blog yako.

Kama umedhamiria blog yako iende mbele basi ni jambo la lazima kuwa unatembelea blogs zenye maudhui ya kufanana nawe ili upate changamoto kuhusu nini cha kufanya na kuandika.

3. Kujibu Maswali au Hoja zinazoulizwa sehemu nyingine ambazo hazijapatiwa Ufumbuzi.

Kama ni mtembeleaji wa blogs/sites nyingine unaweza ku observe ni kipi wafutiliaje wanakihoji na hakijapata majibu au maelezo ii wewe ndo iwe sehemu yako ya kujikusanyia wafuatiliaji kwa kuwapa wanachokihitaji.

4. Kujifunza kutoka kwa waliofanikiwa.

Kama una nia ya dhati ya kufika mbali na Blog yako basi uwe mtu wa kujifunza mara kwa mara toka kwa waliofanikiwa ili nawe utembelea hatua zao katika kukwepa matatizo na kupata mafanikio.

5. Usijiache Peke yako tu, Jichanganye na Bloggers wenzio.

Hii pia ni tatizo kwetu, kwani kuna Bloggers ambao wao wanajiona ndio ma Top, basi hawana muda wa kuwasikiliza hawa wa chini wanaomba nini au ushauri gani wanataka, pia hata kuwawekea link za blogs zao ni shida, pia sisi tunaoanza ku blog tujishirikishe kwa wenzetu ili kukuza traffic na exposure.

Imeandikwa na KAJICHO KIVULI wa JF

0 Comments

Je unamaoni kuhusu makala uliyoisoma dondosha maoni yako hapa