Jinsi ya kuweka matangazo ya adsense katika blog ya kiswahili


Kwa Hali ya Sasa Kumekuwa na Blogs nyingi za Kiswahili ambazo mbali na kujitahidi kupata Akaunti za Adsense bado wanakabiliwa na Changamoto Kubwa ya Matangazo yao Kutooneka, Hii Inatokana na Google Adsense Kuto Support Lugha yetu ya Kiswahili katika Kuratibu Uonekanaji wa Matangazo katika Site Husika. 

Leo Nitakupa Mbinu ambayo Itakufanya Ads ziendelee Kuonekana Japo Una Tumia Lugha ya Kiswahili katika Blog Yako. Binafsi sio Mtaalamu sana wa Mambo ya Codes, Ila nimekubali kujifunza na kujisomesha mtandaoni kwa kadri ya Uwezo wangu. Hivyo Nitakuomba Uridhike na hiki kidogo nitakachokupa leo nawe usisite kuitafuta elimu ya kujazia Sehemu Nyingine kwani ELIMU HAINA MWISHO. 

Japo kuwa sio lazima ujifunze kila kitu Tukirudi katika Mada yetu, Hatua za Kufuata ili Matangazo yaweze Kutokea Katika Site za Lugha ya Kiswahili:- 

1. Ingia kwenye Dashboard yako ya Blogger, Nenda Mpaka kwenye Template, Click Customize Ili Ikupeleke kwenye Edit Css
Baada ya Hapo Nenda Kwenye Tab ya Advanced halafu Add CSS, Hapo Utaingiza Codes za Design Hii kisha Una Apply to Template Halafu Unarudi Kwenye Blogger Template Tena. 

Weka Codes Hizi za Rangi Nyekundu{   </script>  google_language = "en";</script>  
    <meta content='Engish' name='language'/> }  hapo Juu.

2. Hatua ya Pili Unaenda kwenye Blog Dashboard yake unaingia Template halafu Unabonyeza Edit HTML, Ikifunguka Bonyeza mouse yako kwenye code za template kisha bonyeza CTRL+F (Amri ya Kutafuta) Ndani ya Kibox cha Kulia Juu kwenye Codes za HTML utaingiza Codes Hizi <head>  halafu Bonyeza Enter. Chini ya Head Utaingiza Codes Hizi Hapa { <meta content='Engish' name='language'/>  } Kisha Una Save.
Nia Na Madhumuni ni Kuilazimisha Site Yako Kwenye Meta Tags Iitambulishe Kama Ni Site.Blog inayotumia Lugha ya Kiingereza. N.B. Unaweza Ukaweka Mara nying hii Meta Tag kwenye Blog yako though Mimi nakushauri Usizidishe mara 3.

3. Hatua ya Tatu ni Kuandaa Page ya Privacy Policy.
Hapa Utaenda Kwenye Dashboard yako Kisha Utaingia Sehemu ya Pages, Uta Create Page ya Privacy Policy Kisha Utaandika Maneno angalau Paragraphs 4 kuhusiana na Site yako na Vile Ambavyo hautohusika n Comments mbaya kutoka kwako au Wasomoaji wako, Kisha Unai Publish.

Ukishai Publish Unaenda Kwenye Layout katika Dashboard yako Ili Uchague wapi Itakaa Hiyo Page ya Privacy Policy, Ingawa Ikakaa Juu Ni Bora Zaidi.

N.B Post za Nyuma kabla ya Kufanya Trick Hii zinaweza Zisioneshe Ads bali zitaanza Kuonesha zile zitakazokuja baada ya Trick Hii.

Kama Njia Hii Haitaleta Mafanikio Kwako, Ingia Kwenye Ku Edit HTML tena, Kisha Tafuta data:post.body, halafu tafuta Post Footer au Post Footer Line 1 Kisha Uingize yale maneno ya Privacy Policy Humo.


Thanks kwa Kuwa Nami, Kwa Maoni na Ushauri Usisite Kuwasiliana Nami.Niachie maoni yako hapo chini nami nitayafanyia kazi kwa kukupa majibu kadri nitakavyofahamu maswali yako.

5 Comments

  1. Habari nimejaribu hizi code na nimetengeneza Privacy policy lakini bado inakataa na nimejaribu kupast maneno ya privacy pale kwa chini yakini bado inakataa. Please nisaidie.

    ReplyDelete
  2. 🔥🔥 Hakika hutojuta kujiunga kwenye magroup haya👇👇

    Group la kazi na Ajira
    https://t.me/TanzaniteMedia1
    Njia za kutengeneza pesa mtandaoni 👇👇
    https://t.me/WapambanajiForum

    Blog ya Kutengeneza pesa mtandaoni kwa kutumia Smartphone Yako👇👇
    https://jovinskills.blogspot.com

    Blog inakupa Update za Nafasi za kazi,Ajira na fursa mbalimbali 👇👇
    https://tanzanitemedia1.blogspot.com

    ReplyDelete
  3. Hey umewezaje kulink blogger na adsence

    ReplyDelete

Je unamaoni kuhusu makala uliyoisoma dondosha maoni yako hapa