JE' ADSENSE WANATAKA KUKUBALI MATANGAZO YAO KATIKA BLOG ZA KISWAHILI?

As salaam aleikum ndugu zangu kwa wale blogger wa kongwe na wale wachanga ni kipindi kirefu tumesikia kuhusu neno adsense lakini kumekuwa hakuna Tija ya kulisikia tu neno Adsense, sababu hata baada ya kulisikia na kulijua kumekuwa ni vigumu kunufaika nalo kutokana na masharti yao.
Leo katika uchambuzi huu tuelewe kwanini Tunafikiri adsense wanaweza kukiweka kiswahili kati ya lugha zinazosapoti katika matangazo yao? 

Katika masiku ya hizi karibuni kampuni ya google imeboresha mtandao wake na huduma zake zote kwa ujumla kama kubadilisha muonekano wa dashbodi ya blogger.com, adword, adsense, youtube, google map, na hata adsense pamoja na mfumo wa upakiaji app wa google console, Lakini ukiangalia kipaumbele walichokipa kiswahili katika program zao ni kubwa mno kwa wale watumiaji wa google translate watakuwa wameona hili.

Kwa sasa lugha ya  Kiswahili imepata pendeleo la kutafsiriwa bila hata kuwa na muunganisho  wa data,hii ni fursa nzuri hasa pale utakapokuwa huna kifurushi.

Na kwa upande wa adsense ilikuwa kipindi cha nyuma ukifungua blog kisha kabla hujaifikia dashbodi ya blog ukachagua lugha ya kiswahili ndio iwe lugha mama ya blog yako google walikuwa wanakiondosha kipengele cha mapato katika blog yako.
 Lakini kwasasa kipengele hicho kinawekwa na google wenyewe hata kama utafungua blog yako kwa lugha ya kiswahili mwanzo mwisho, hii ni wazi siku za usoni blogger wanaotumia lugha ya kiswahili katika kuendesha blog zao wataanza kunufaika na adsense.

Hayo ndio machache kati ya mengi tuliyokuandalia siku ya leo endelea kuwa nasi ili kufahamu zaidi kuhusu ADSENSE

0 Comments

Je unamaoni kuhusu makala uliyoisoma dondosha maoni yako hapa