Twitter yazifunga zaidi ya akaunti 3,000 kutoka nchi 6, mbili za Afrika Mashariki

Twitter  hapo jana siku ya Alhamisi imesema kuwa imeondoa akaunti 3,465 zinazofanya kazi kama “operesheni za habari zinazoungwa mkono na serikali” ambazo ilizihusisha na nchi sita: Uchina, Mexico, Urusi, Tanzania, Uganda na Venezuela.


Nchini Uganda, Twitter iliondoa mtandao wa akaunti 418 “zilizokuwa zikishiriki katika shughuli zisizo halali” za kumuunga mkono Rais Yoweri Museveni na chama chake, National Resistance Movement.


Takriban akaunti 268 pia zilifungwa nchini Tanzania baada ya kupatikana kuwasilisha ripoti za nia mbaya kwenye Twitter.


Mexico – 276 akaunti

China – 2,160 akaunti

Urusi – 66 akaunti

Tanzania – 268 akaunti

Uganda – 418 akaunti

Venezuela – 277 akaunti

wasiliana nami

0 Comments

Je unamaoni kuhusu makala uliyoisoma dondosha maoni yako hapa